OKWI NA NIYONZIMA KUIMALIZA YANGA
Mayanja ameiambia SIMBA FC, mchezo dhidi ya Yanga, utakuwa mgumu lakini kuwa na wachezaji wazoefu kwenye kikosi chao kama Emmanuel Okwi na Haruna Niyonzima, kunatamaliza mchezo huo mapema kwa wao kupata ushindi.
“Tunaingia kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii, tukijivunia Okwi na Niyonzima hata kama wasipofunga lakini uwepo wao ni ushindi tosha kwa Simba kwasababu asilimia kubwa ya wachezaji wa Yanga na mashabiki wao wanawaogopa wachezaji hao,”amesema Mayanja.
Kocha huyo amesema wanakiu ya kushinda pambano hilo ili kuanza vyema msimu mpya wa ligi ya Vodacom na kubeba Ngao ya Jamii ni ishara nzuri kwao kwani kutawaongezea ari ya kucheza kwa kujituma na kutimiza kile ambacho wanakihitaji.
Pambano hilo la watani wa jadi linapigwa kesho uwanja wa Taifa Dar es Salaam, na Simba wanapewa nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi kutokana na aina ya wachezaji iliyowasajili msimu huu.

Comments
Post a Comment