SIMBA HAITAJUTA KUNISAJILI

Kwa namna Gyan alivyoonyesha uwezo, ni lazima wapangue safu ya ushambuliaji na kuunda kombinesheni mpya kwa mujibu wa Jackson Mayanja 
 
Mshambuliaji mpya wa Simba raia wa Ghana, Nicholas Gyan, aliyesajiliwa msimu huu akitokea klabu ya Ebusua Dwarfs ya Ligi Kuu Ghana amesema atahakikisha ana funga kila mechi atakayopewa nafasi na mwalimu.

Gyan juzi alifungua akaunti yake ya magoli baada ya kufanikiwa kufunga goli moja dhidi ya Hard Rock kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Mghana huyo allifanya mahojiano na gazeti la Mwanaspoti alisema kiu yake ni kuona anafunga kila mechi.

“Baada ya kufanya vizuri katika ligi ya nyumbani Ghana, sasa nimekuja Simba ili kuendeleza kasi yangu ya ufungaji, Simba haitajuta kunisajili,” alisema hivyo Mghana huyo.

Gyan anatarajia kucheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu wikendi hii dhidi ya Waoka mikatae wa Dar es salaam, Azam.

Comments

Popular posts from this blog

OKWI NA NIYONZIMA KUIMALIZA YANGA

OKWI WE ACHA TU......