Posts

Showing posts from August, 2017

OMOG""SIMBA MOTO ULE ULE

Image
Kocha wa Simba amesema wamepania kuendeleza wimbi lao la ushindi katika michuano ya ligi kuu hivyo asingependa kutoa mapumziko kwa baadhi ya wachezaji    Kocha mkuu wa Simba Joseph Omog amesema kikosi chake kitaendelea na mazoezi kwa wachezaji ambao hawapo timu ya Taifa lengo likiwa ni kulinda viwango vyao. Omog ameiambia SIMBA FC ameona afanye hivyo ili viwango vya wachezaji wake visishuke katika kiwango walichonacho kwa sasa ili waweze kuendeleza moto wao wakati ligi itakapoendelea Septema 5. "Tupo kwenye kiwango bora kwa sasa kuwapa wachezaji mapumziko ni sawa na kushusha viwango vyao na kupoteza ari ya kimchezo waliokuwa nayo hivi sasa hivyo ni bora tukaendelea na mazoezi  mpaka Septemba 3 wakati kiksi kitakapokamilika," amesema Omog. Kocha huyo raia wa Cameroon amesema wamepania kuendeleza wimbi lao la ushindi katika michuano ya ligi kuu hivyo asingependa kutoa mapumziko kwa baadhi ya wachezaji ipi kutimiza kile walichokipanga. A...

OKWI WE ACHA TU......

Image
Simba wameonyesha ishara njema ya kupata mafanikio Ligi Kuu Bara msimu huu baada ya kuanza ligi kwa ushindi wa mabao 7 Emmanuel Okwi akiongeza sherehe.   Simba SC imeanza Ligi Kuu Bara na moto mkali, baada ya kuichapa mabao 7-0 Ruvu Shooting jioni ya leo Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Mshambuliaji Mganda, Emmanuel Arnold Okwi ameonyesha msimu huu amedhamiria kurudi kivingine katika Ligi Kuu, baada ya kufunga mabao manne na kuseti moja katika ushindi huo mnono. Mabao mengine ya Wekundu wa Msimbazi, walio chini ya kocha Mkameruni, Joseph Marius Omog anayesaidiwa na Mganda, Jackson Mayanja yamefungwa na Shiza Ramadhani Kichuya, Juma Luizio Ndanda na Erasto Edward Nyoni. Okwi alifungua sherehe za mabao dakika ya 18 akimchambua kipa Bidii Hussein baada ya pasi ya Muzamil Yassin na bao la pili akafunga dakika ya 22 baada ya kuwachambua mabeki ndani ya boksi kufuatia pasi ya kiungo Mnyarwanda, Haruna Niyonzima. Okwi akakamilisha hat trick yake dakik...

OKWI NA NIYONZIMA KUIMALIZA YANGA

Image
Kocha msaidizi wa Simba amesema anamatumaini ya kikosi chake kuibuka na ushindi mnono dhidi ya mahasimu wao Yanga katika pambano la Ngao ya Jamii    Kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja, amesema wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanaifunga Yanga kesho na kutwaa taji la Ngao ya Jamii kama ambavyo wamekusudia. Mayanja ameiambia SIMBA FC, mchezo dhidi ya Yanga,  utakuwa mgumu lakini kuwa na wachezaji wazoefu kwenye kikosi chao kama Emmanuel Okwi na Haruna Niyonzima, kunatamaliza mchezo huo mapema kwa wao kupata ushindi. “Tunaingia kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii, tukijivunia Okwi na Niyonzima hata kama wasipofunga lakini uwepo wao ni ushindi tosha kwa Simba kwasababu asilimia kubwa ya wachezaji wa Yanga na mashabiki wao wanawaogopa wachezaji hao,”amesema  Mayanja. Kocha huyo amesema wanakiu ya kushinda pambano hilo ili kuanza vyema msimu mpya wa ligi ya Vodacom na kubeba Ngao ya Jamii ni ishara nzuri kwao kwani kutawaongezea ari ya k...

MACHO YOTE KWA NIYONZIMA NA AJIBU

Image
Pambano lililosubiriwa kwa siku nyingi limefika, ni Simba dhidi ya Yanga katika mechi ya Ngao ya Jamii, Niyonzima na Ajibu wakikabili timu zao za kale    Miamba ya soka Tanzania Yanga na Simba inakutana kesho Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, ukiwa ni mchezo wa Ngao ya Jamii ambao unaashiria kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom. Presha imekuwa kubwa kwa pande zote mbili, huku Simba wakiwa na matumaini makubwa ya kushinda mchezo huo kutokana na usajili ambao wameufanya msimu huu kwa kusajili nyota wenye majina makubwa. Mara ya mwisho timu hizo kukutana ilikuwa ni Februari mwaka huu, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1, kwahiyo usajili walioufanya msimu huu pamoja na ushindi walioupata mwisho kumewajengea imani mashabiki wa Simba wakiamini rekodi hiyo itaendelea tena kesho. Kuelekea mchezo huo Yanga wameendelea kujifua kwa kutumia nyota waliosajili kipindi hiki cha usajili ingawa mashabiki wao wameonyesha hofu kutokana na u...