Posts

Showing posts from September, 2017

SIMBA HAINA HOFU KUCHEZA CHAMANZI

Image
Kocha msaidizi wa Simba Jackson Mayanja, amesema kucheza uwanja wa Chamaz ni nafasi kwa wachezaji wao kucheza bila msaada wa mashabiki    Uongozi wa klabu ya Simba umesema hauhofii kitu chochote kuhusiana na Bodi ya Ligi kubadili ratiba na kuipanga mechi yao na Azam kupigwa uwanja wa Azam Complex Chamazi Jumamosi. Kocha msaidizi wa Simba Jackosn Mayanja, ameiambia SIMBA FC, ni mchezo mkubwa lakini kucheza uwanja wa Chamazi siyo kikwazo cha wao kushindwa kuendeleza kasi yao waliyoanza nayo. “Tunaheshimu maamuzi ya bodi ya ligi na Simba tumejipanga kuhakikisha tunashinda popote pale tunapocheza siyo uwanja wa Uhuru au Taifa peke yake nahiyo inatokana na ubora wa kikosi tulichonacho msimu huu,”amesema Mayanja. Kocha huyo amesema mabadiliko hayo yatawajenga wachezaji wao kucheza kwa kujituma bila sapoti ya karibu kutoka kwa mashabiki wao ambao wamekua wakijaa kwa wingi uwanjani kuwashangilia. Amesema kuna safari wanakwenda mikoani, hujikuta kama ...

SIMBA HAITAJUTA KUNISAJILI

Image
Kwa namna Gyan alivyoonyesha uwezo, ni lazima wapangue safu ya ushambuliaji na kuunda kombinesheni mpya kwa mujibu wa Jackson Mayanja    Mshambuliaji mpya wa Simba raia wa Ghana, Nicholas Gyan, aliyesajiliwa msimu huu akitokea klabu ya Ebusua Dwarfs ya Ligi Kuu Ghana amesema atahakikisha ana funga kila mechi atakayopewa nafasi na mwalimu. Gyan juzi alifungua akaunti yake ya magoli baada ya kufanikiwa kufunga goli moja dhidi ya Hard Rock kwenye mechi ya kirafiki iliyochezwa Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Mghana huyo allifanya mahojiano na gazeti la Mwanaspoti alisema kiu yake ni kuona anafunga kila mechi. “Baada ya kufanya vizuri katika ligi ya nyumbani Ghana, sasa nimekuja Simba ili kuendeleza kasi yangu ya ufungaji, Simba haitajuta kunisajili,” alisema hivyo Mghana huyo. Gyan anatarajia kucheza mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu wikendi hii dhidi ya Waoka mikatae wa Dar es salaam, Azam.

AZAM FC YAFURAHIA MECHI ZAKE NA SIMBA KUPELEKWA CHAMANZI

Image
Mabadiliko ya ratiba mpya ya Ligi Kuu yanaonyesha kuwa mechi zote za Azam FC za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga zitafanyika Uwanja wa Azam Complex.   Klabu ya Azam FC imefuraishwa na taarifa za shirikisho la mpira TFF kuruhusu mechi zao dhidi ya  Simba na Yanga kufanyika kwenye uwanja wao wa Chamanzi. Kwa mara ya kwanza mechi ya Azam na Simba itafanyika katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Jumamosi hii Septemba 9. " Ni furaha tupu ndani ya viunga vya Azam Complex kwenye makao makuu ya Klabu BIngwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuiruhusu timu hiyo kutumia uwanja huo kwa mara ya kwanza kwenye mechi zake za nyumbani dhidi ya Simba na Yanga. waliandika hivyo kupitia kwenye mtandao wao wa klabu.