SIMBA HAINA HOFU KUCHEZA CHAMANZI
Kocha msaidizi wa Simba Jackosn Mayanja, ameiambia SIMBA FC, ni mchezo mkubwa lakini kucheza uwanja wa Chamazi siyo kikwazo cha wao kushindwa kuendeleza kasi yao waliyoanza nayo.
“Tunaheshimu maamuzi ya bodi ya ligi na Simba tumejipanga kuhakikisha tunashinda popote pale tunapocheza siyo uwanja wa Uhuru au Taifa peke yake nahiyo inatokana na ubora wa kikosi tulichonacho msimu huu,”amesema Mayanja.
Kocha huyo amesema mabadiliko hayo yatawajenga wachezaji wao kucheza kwa kujituma bila sapoti ya karibu kutoka kwa mashabiki wao ambao wamekua wakijaa kwa wingi uwanjani kuwashangilia.
Amesema kuna safari wanakwenda mikoani, hujikuta kama wanyonge kwa kukosa sapoti hivyo kucheza uwanja wa Chamazi msimu huu yeye anaamini kutakuwa na faida kwao ya kucheza bila kuhitaji sapoti ya mashabiki.
Ratiba iliyofanyiwa marekebisho ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara, imetoka jana imeonyesha timu za Simba na Yanga ambazo zilikuwa hazichezi uwanja wa Azam Complex sasa kuanzia msimu huu zitakwenda kucheza huko pindi zinapopambana na wenyeji Azam FC.
Comments
Post a Comment